Utangulizi: Orodha Kamili ya Masomo ya Diploma ya Famasi Tanzania – Mwaka wa Kwanza hadi wa Tatu
Taaluma ya famasi ni mhimili muhimu katika sekta ya afya, ikihusisha uzalishaji, usambazaji, matumizi sahihi ya dawa na ushauri wa kitaalamu kwa wagonjwa. Kwa kutambua umuhimu huu, vyuo mbalimbali nchini Tanzania vinatoa kozi ya Diploma ya Famasi chini ya usimamizi wa NACTVET ili kuandaa wataalamu wenye weledi, maadili, na ujuzi wa kati unaohitajika katika mfumo wa afya.
Kozi ya Diploma ya Famasi huchukua muda wa miaka mitatu, ambapo kila mwaka hugawanyika katika Semester I na II. Masomo haya yameundwa kitaalamu ili kumpa mwanafunzi mchanganyiko wa nadharia, mafunzo kwa vitendo (practical), na stadi za kazi (industrial training) zinazohitajika katika mazingira halisi ya kazi.
Katika makala hii, utapata:
- Orodha ya masomo ya kila mwaka, kuanzia mwaka wa kwanza hadi wa tatu
- Mgawanyo wa masomo kwa kila semester
- Mwanga wa kile unachopaswa kukitarajia kama mwanafunzi wa famasi
Iwe wewe ni mwanafunzi unayetarajia kujiunga, mzazi unayetaka kumsaidia mtoto wako kuchagua kozi sahihi, au mdau wa afya unayetaka kujua mtaala wa elimu ya kati ya famasi nchini – makala hii ni rejea bora na ya kuaminika kwa ajili yako.
MWAKA WA KWANZA | |||
Na. | Jina la somo | Semester (Mhula) | Somo linahusu |
1 | Dispensing | I | Utoaji sahihi wa dawa |
2 | Disease Control and prevention | I | Magonjwa ya binadamu, matibabu na njia za kuzuia |
3 | Human Anatomy and Physiology | I | Mwili wa binadamu ua utendaji kazi wake (seli, Mifupa, Ogani n.k |
4 | Pharmaceutical Dosage Forms | I | Aina za dawa na mifumo yake, jinsi ya kutumia n.k |
5 | Pharmaceutical Calculations | I | Hesabu za kifamasia, kama vile dose n.k |
6 | Communication Skills | I | Ujuzi katika mawasiliano |
7 | Basic Computer Applications | I | Ujuzi katika kompyuta |
8 | Laws and Ethics in Pharmacy | II | Miiko na Maadili katika Taaluma ya Famasi |
9 | Compounding of pharmaceutical liquid preparations | II | Jinsi ya kutengeneza dawa za maji |
10 | Pharmaceutical Inorganic Chemistry | II | Metali na Simetali na kazi zake katika Ufamasia |
11 | Basic pharmacology | II | Makundi ya dawa, matumizi yake n.k |
12 | Medical Stores Keeping | II | Jinsi ya kutunza na kupanga dawa eneo la store |
13 | Pharmacy Practice | II | Mafunzo kwa vitendo (Field) |
MWAKA WA PILI | |||
Na. | Jina la somo | Semester (Mhula) | Somo linahusu |
1 | Medicines and medical supply management | I | Jinsi ya kutunza kugawa, kununua dawa kwa wazabuni |
2 | Law and policies in Pharmacy | I | Sheria na sera kwenye famasi |
3 | Pharmaceutical Microbilogy | I | Wadudu wanaosababisha magonjwa kwa binadamu |
4 | Pharmacology and Therapeutics | I | Makundi ya dawa Jinsi zinavyofanya kazi mwili n.k |
5 | Rational Use of Medicines | I | Matumizi sahihi ya dawa n.k |
6 | Pharmaceutical organic Chemistry | I | Umhumi wa Organic Compuound kwenye Famasi, namna ya kugungundua dawa n.k |
7 | Quality assurance of pharmaceutical products | II | Udhibiti wa ubora wa dawa |
8 | Pharmaceutics theory and compounding | II | Jinsi ya kutengeneza dawa za mafuta (za kupakaa) |
9 | Health information Management | II | Utunzaji wa taarifa za Afya |
10 | Basic pharmacognosy | II | Mimea tiba na magonjwa yake, Namna ya kutengeneza |
11 | Pharmacy Practice | II | Mafunzo kwa vitendo (Field) |
MWAKA WA TATU | |||
Na. | Jina la somo | Semester (Mhula) | Somo linahusu |
1 | Leadership and Management | I | Uongozi katika nyanja mbalimbali |
2 | Counselling and Guidance skills | I | Ujuzi katika kumshauri mgonjwa kwenye hali mbali mbali |
3 | Pharmaceutical Production | I | Jinsi ya kutengeneza dawa za vidonge kiwandani |
4 | Health and Medicines Policy | I | Sera za Afya na Dawa |
5 | Health Financing | I | Mifumo ulipia wa huduma za afya, Bima n.k |
6 | Basic Pharmacotherapy | I | Matibu ya Magonjwa kwa kutumia dawa, namna ya kuchagua dawa sahihi |
7 | Basic Veterinary pharmacology | I | Dawa baadhi zinatumika kwa wanyama wafugwao |
8 | Pharmaceutical Public Health | II | Uteteaji na uchocheaji wa kuboresha afya ya jamii |
9 | Entrepreneurship | II | Ujasiriamali katika Famasi |
10 | Operational Research | II | Kufanya utafiti katika sekata za Afya |
11 | Monitoring and Evaluation of Medicines Use | II | Ufauatiliaji wa matumizi ya dawa, jinsi dawa inavyotengezwa mpaka kufukia jamii |
12 | Pharmacy Practice | II | Mafunzo kwa vitendo (Field) |
Mapendezo ya Mhuriri;
- Orodha ya Vyuo vinavyotoa kozi ya diploma ya Famasi Tanzania.
- Jinsi ya kutuma maombi Kusoma Diploma ya Famasi.
Hitimisho!
Kozi ya Diploma ya Famasi Tanzania imeundwa kwa umakini mkubwa ili kuwajengea wanafunzi msingi imara wa kitaaluma na vitendo katika taaluma ya afya. Kupitia orodha hii ya masomo iliyopangwa kwa kila mwaka na kila semester, wanafunzi wanapata mwanga wa kile wanachotarajia kujifunza, hali inayowawezesha kuwa na maandalizi mazuri ya kitaaluma na kisaikolojia.
Uelewa wa muundo wa masomo haya si tu unasaidia katika kupanga ratiba za kujisomea, bali pia huwasaidia wanafunzi kujiwekea malengo ya muda mfupi na mrefu katika taaluma yao ya famasi. Hii pia ni nyenzo muhimu kwa wazazi, walezi, na mashirika ya elimu kutathmini ubora na umakini wa mitaala inayotolewa na vyuo vinavyotoa kozi hii.
Ikiwa unalenga kuingia katika sekta ya afya kwa ngazi ya kati, Diploma ya Famasi ni miongoni mwa kozi zenye fursa pana za ajira na maendeleo ya kitaaluma. Hakikisha unafanya maamuzi sahihi mapema, ukianza kwa kuielewa kozi yako kuanzia msingi – kama ulivyojifunza kupitia makala hii.