Tazama Vyuo Vinavyotoa Diploma ya Famasi Tanzania 2025/2026

Admin

Vyuo Vinavyotoa Diploma ya Famasi Tanzania – Fursa ya Kitaaluma na Ajira

Katika dunia ya sasa, taaluma ya famasi si tu kuhusu kugawa dawa, bali ni sehemu muhimu ya mfumo wa afya unaohitaji weledi, uadilifu, na maarifa ya kisayansi. Tanzania ikiwa na ongezeko la mahitaji ya wataalamu wa afya, vyuo mbalimbali nchini vimeanzisha kozi ya Diploma ya Famasi (Pharmaceutical Sciences) ili kukidhi hitaji hilo.

Kozi hii huwapa wanafunzi maarifa ya msingi kuhusu dawa, utengenezaji wake, usambazaji, matumizi sahihi, na ushauri kwa wagonjwa – ikiwajengea msingi thabiti wa kitaaluma na kijamii. Kwa wahitimu wa kidato cha nne wanaotamani kuingia kwenye sekta ya afya kwa ngazi ya kati, diploma ya famasi ni chaguo sahihi na lenye matarajio makubwa ya ajira ndani na nje ya nchi.

Katika makala hii, utajifunza kuhusu:

  • Orodha ya vyuo vya serikali na binafsi vinavyotoa Diploma ya Famasi nchini Tanzania
  • Sifa za kujiunga
  • Namna ya kutuma maombi

Ikiwa unatafuta fursa ya kitaaluma yenye mwelekeo mzuri wa ajira, basi endelea kusoma – huenda hapa ndipo mwanzo wa safari yako ya mafanikio katika sekta ya afya.

Orodha ya Vyuo 36 Vinavyotoa kozi ya diploma ya Famasi Tanzania.

S/NJina la Taasisi ya MafunzoMkoaUmiliki
1Muhimbili University of Health and Allied SciencesDar es SalaamSerikali
2Catholic University of Health and Allied SciencesDar es SalaamSerikali
3St. John’s University of TanzaniaNjombeBinafsi
4City College of Health and Allied SciencesDodomaBinafsi
5Kilimanjaro School of PharmacyKilimanjaroBinafsi
6Ruaha University CollegeIringaBinafsi
7Royal Training InstituteMbeyaBinafsi
8St. Peters College of Health ScienceDar es SalaamBinafsi
9Kampala International UniversityDar es SalaamBinafsi
10Njombe Health Training InstituteNjombeBinafsi
11St. John College of Health ScienceMbeyaBinafsi
12Spring Institute of Business and Health ScienceDar es SalaamBinafsi
13University of Dodoma (UDOM)DodomaSerikali
14Tandabui Health CollegeMwanzaBinafsi
15Kigamboni City CollegeDar es SalaamBinafsi
16Paradigm Pharmacy CollegeDar es SalaamBinafsi
17Kahama College of Health SciencesKahamaBinafsi
18St. Joseph University in TanzaniaDar es SalaamBinafsi
19St. Fransic University of Health and Allied SciencesIfarankaBinafsi
20Mtwara Clinical Officer Training CenterMtwaraSerikali
21St. Maximillian Colbe Health CollegeTaboraBinafsi
22DECCA College of Health and Allied SciencesDodomaBinafsi
23St. Aggrey CollegeMbeyaBinafsi
24Musoma Utalii CollegeTaboraBinafsi
25Blue Pharma College of Health SciencesSingidaBinafsi
26Apple Valley College of Health SciencesDar es SalaamBinafsi
27Top One CollegeSongeaBinafsi
28K’s Royal Training InstitutionMbeyaBinafsi
29Green Bird CollegeKilimanjaroBinafsi
30Karagwe Institute of Health and Allied SciencesKaragweBinafsi
31West Tanganyika CollegeKigomaBinafsi
32Mbeya College of Health SciencesMbeyaSerikali
33Lugarawa Health Training InstituteNjombeBinafsi
34Northern College of Health and Allied SciencesKilimanjaroBinafsi
35Peramiho Institute of Health and allied sciencesRuvumaBinafsi
36Marian University College (Mar)PwaniBinafsi

SOMA PIA >>> ORODHA YA VYUO VIKUU TANZANIA HAPA

Sifa kujiunga Diploma ya Famasi Nchini Tanzania

Sifa za msingi (kwa CSEE/Kidato cha Nne):

  • Ufaulu katika masomo manne yasiyo za dini
  • Angalau alama ya “D” katika Kemia na Baiolojia
  • Alama ya “D” katika matatu yasioyodini, Aidha ufaulu katika somo the kingereza na hisabati inakupa sifa za ziada za kuendelea kusoma shahada siku za usoni

Jinsi ya Kutuma Maombi ya Diploma ya Famasi Kupitia Mfumo wa CAS – NACTVET

Mfumo wa CAS (Central Admission System) unaosimamiwa na NACTVET hutumika na waombaji wanaotaka kujiunga na vyuo vya afya, mafundi sanifu, ualimu wa diploma, n.k. kwa ngazi ya Certificate (Astashahada) na Diploma (Stashahada).

1. Tembelea Tovuti Rasmi ya CAS – NACTVET

2. Bonyeza Sehemu ya “Start Application” au “New Applicant”

  • Kwa mara ya kwanza, jisajili kwa kutumia:
    • Jina lako kamili
    • Email ya kuaminika
    • Namba ya simu
    • Nambari ya mtihani wa NECTA (CSEE)
  • Baada ya kujisajili, utapata jina la mtumiaji (username) na neno la siri (password)

3. Ingia kwenye Akaunti Yako

  • Tumia username na password kuingia kwenye akaunti
  • Mfumo utaonesha taarifa zako za NECTA (kwa waliomaliza kidato cha nne)
  • Hakikisha taarifa zote ni sahihi

4. Chagua Kozi ya Kuomba – Diploma ya Famasi

  • Katika menyu ya kozi, tafuta “Diploma in Pharmaceutical Sciences”
  • Chagua chuo/vyuo vinavyotoa kozi hiyo
    • Unaweza kuchagua hadi vyuo vitano (5) tofauti

5. Jaza Taarifa Zilizobaki

  • Taarifa binafsi: tarehe ya kuzaliwa, makazi, jinsia
  • Pakia picha ya pasipoti (passport size)
  • Hakikisha kila sehemu umejaza ipasavyo

6. Lipa Ada ya Maombi (Application Fee)

  • Ada ni TSh 10,000
  • Mfumo utakupa control number
  • Lipa kupitia:
    • M-Pesa / Tigo Pesa / Airtel Money
    • Benki ya NMB, CRDB, au benki nyingine

Mfano wa Kulipa kwa M-Pesa:

Piga *150*00# → LIPA kwa M-Pesa → Malipo ya Serikali → Ingiza control number → Kiasi → Namba ya siri

7. Thibitisha na Tuma Maombi

  • Baada ya kulipa, nenda tena kwenye akaunti yako ya CAS
  • Hakikisha taarifa zote ni sahihi
  • Thibitisha (Submit) maombi yako

8. Subiri Majibu ya Uchaguzi

  • Orodha ya waliochaguliwa hutangazwa kupitia:
    • Akaunti yako ya CAS
    • Tovuti ya NACTVET
    • Simu (SMS) au barua pepe
  • Ukichaguliwa, utapata Joining Instructions kutoka chuo husika
Leave a Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *