Juni 6, 2025 – Dodoma: Utangulizi muhimu!
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mheshimiwa Mohamed Mchengerwa, ametangaza rasmi majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano na Vyuo vya Elimu ya Ufundi kwa mwaka wa masomo 2025/2026.
TAMISEMI imetangaza rasmi majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano mwaka 2025. Orodha hii inahusisha wanafunzi wote waliomaliza mtihani wa kidato cha nne (CSEE) 2024 na kufuzu kwa ajili ya kuendelea na elimu ya sekondari kidato cha tano katika shule mbalimbali za serikali Tanzania Bara.
Wanafunzi sawa na asilimia wamechaguliwa Kujiunga na masomo ya kidato cha tano ambapo wamechaguliwa kijinga na vyuo vya elimu ya ufundi na ualimu
Jumla ya Wanafunzi 214,141 wakiwemo wasichana 97,517 na wavulana 116,624 wameonekana wana sifa ya Kujiunga na masomo ya kidato cha tano na wengine vyuo vya katiikijumlisha Wanafunzi 1028 wenye uhitaji maalum
Jinsi ya Kuangalia Shule Walizopangiwa Kidato cha Tano 2025 Hatua kwa Hatua
Ili kuangalia shule uliopangiwa, fuata hatua hizi rahisi:
- Tembelea tovuti rasmi ya NECTA: Kwa kuwa NECTA ndio chombo kinachosimamia mitihani na mipangilio ya wanafunzi, tovuti yao rasmi ni chanzo cha habari zilizo sahihi. Anza kwa kuingia www.necta.go.tz.
- Tafuta sehemu ya ‘Shule Walizopangiwa Kidato cha Tano 2025’: Mara kwenye tovuti, angalia sehemu ya matangazo au matokeo.
- Ingiza taarifa zako: Fungua sehemu inayolazimisha kuingiza taarifa kama jina kamili la mwanafunzi na namba ya mtihani.
- Bonyeza kitufe cha ‘Tafuta/Shule Walizopangiwa’: Taarifa za shule zitajitokeza mara moja.
- Hifadhi au chapisha taarifa: Ni vyema kuhifadhi au kuchapisha orodha ya shule kwa ajili ya kumbukumbu na juhudi za baadaye.
BOFYA HAPA KUONA ORODHA YA WANAFUNZI WALIOPANGWA KWENDA SHULE MOJA
OFISI YA RAIS – TAMISEMI
UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2025
CHAGUA MKOA ULIKOSOMA
ARUSHA | DAR ES SALAAM | DODOMA |
GEITA | IRINGA | KAGERA |
KATAVI | KIGOMA | KILIMANJARO |
LINDI | MANYARA | MARA |
MBEYA | MOROGORO | MTWARA |
MWANZA | NJOMBE | PWANI |
RUKWA | RUVUMA | SHINYANGA |
SIMIYU | SINGIDA | SONGWE |
TABORA | TANGA |
Faida za Kujua Shule Walizopangiwa Mapema
- Kurahisisha maandalizi ya kupata masomo na makazi.
- Kupunguza msongo wa mawazo kwa wazazi na wanafunzi.
- Kuwezesha wanafunzi kuanza kupanga mipango ya masomo na maisha ya shule mpya.
- Kupunguza hatari ya upotevu wa taarifa potofu na udanganyifu.
Hitimisho
Kupata taarifa sahihi kuhusu shule walizopangiwa kidato cha tano ni jambo la msingi kwa kila mwanafunzi. Kwa kufuata hatua tulizozitoa, unaweza kwa urahisi kujua shule uliopangiwa kwa mwaka 2025 na kuanza maandalizi kwa wakati. Kumbuka kutumia vyanzo rasmi ili kuhakikisha unapata habari za ukweli na za kuaminika.
Kwa habari zaidi na usaidizi, tembelea tovuti rasmi za Bodi ya Mitihani Tanzania (NECTA) na Wizara ya Elimu.